Day: September 27, 2018
Kuingiliwa Majukumu kwamtimua Kocha Sudan Kusini.
Ahcene Ait Abdelmalek amebwaga manyanga kuifundisha timu ya Taifa ya Sudani Kusini kutokana na kuingiliwa na chama cha soka kuhusu uteuzi wa Kikosi. Kocha huyo wa Kijerumani mwenye asili ya Algeria alisaini mkataba wa miaka miwili na chama cha soka Sudan Kusini (SSFA) kuifundisha timu hiyo March mwaka huu. “Wananiingilia majukumu nakusema mchezaji huyu anapaswa kucheza, huyu hapaswi kucheza au kwa nini huyu achezi?” alisema hayo katika mahojiano. Lakini SSFA wakakanusha haraka madai ya Kocha huyo wakidai watatoa taarifa kuhusu hilo muda si mrefu. Zaidi Kocha huyo amesema anaamini Timu…
Read MoreAFISA USTAWI MATATANI KWA KUMTAJA RC HAPI KUTAFUNA HELA ZA WENYE ULEMAVU
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally hapi amemsimamisha kazi na kumtupa rumande saa 48 afisa ustawi wa jamii wa manispaa ya Iringa Bw. Sitta kwa kosa la kuwaambia chama cha viziwi kuwa manispaa hiyo haiwezi kuwasaidia kwa sasa kwasababu fedha nyingi zimetumika kwenye ziara za mkuu wa mkoa
Read MoreHawa Ndio Nyota 30 tayari kuivaa CAPE VERDE.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike ametangaza Kikosi cha wachezaji 30 watakaongia kambini kujiandaa na mchezo wa kufuzu AFCON 2019 dhidi ya Cepe Verde. MAGOLIKIPA: 1 Aishi Manula (Simba) 2 Beno Kakolanya (Yanga) 3 Mohamed Abdulahm (JKT Tanzania) WALINZI: 4 Hassan Kessy (Nkana) 5 Shomari Kapombe (Simba) 6 Salum Kimenya (Prisons) 7 Gadiel Michael (Yanga) 8 Paulo Ngalema (Lipuli) 9 Ally Sonso(Lipuli), 10 Aggrey Morris (Azam), 11 David Mwantika (Azam), 12 Abdallah Kheri (Azam) 13 Kelin Yondani (Yanga), Andre Vicent (Yanga), 14 Abdi Banda (Baroka) 15 Andrew Vincent…
Read MoreALIYEWAHI KUWA RAISI WA CHAMA KIKUU CHA UPINZANI ABWAGA MANYANGA AANZISHA CHAMA CHAKE
Aliyewahi kuwa rais wa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda cha FDC, Jenerali Mugisha Muntu amekihama rasmi chama hicho na kutangaza kwamba ataanzisha chama kipya hivi karibuni. Hatua hiyo ya Muntu inafuatia kushukiwa na baadhi ya wanachama wa FDC, kuwa pandikizi la chama tawala. Shutuma hizo amezikanusha vikali.
Read MoreUS na China kunaweza kumuongezea umaarufu AJ.
Bondia wa uzito wa juu kutoka China Zhang Zhilei anaamini umaarufu wa bingwa wa Dunia Anthony Joshua utazidi endapo atapambana nje ya Ulaya kama America na China. Wenye kumbukumbu Zhilei alicharanzwa katika robo finali na kutupwa nje ya Michuano ya Olimpiq pale London 2012 akipigwa na Joshua ambaye alisonga mbele nakuchukua medali ya Dhahabu. Miaka 6 baadae Zhilei hajapigwa katika mapambano 19 ya kulipwa na akijiendeleza zaidi katika Jiji la New York lakini pambano lake lijalo litafanyika China siku ya Kesho na amini atamsaidia Joshua kukuza soko lake na umaarufu…
Read MoreUpdate kutoka Ukara: MV Nyerere
Jitihada za kukiinua kutoka kwenye maji kivuko cha feri ya mv Nyerere zinaendelea ambapo hadi sasa kivuko hicho kimeripotiwa kuanza kuibuka hasa upande wa mbele. #Updatekutoka ukara
Read MoreRAISI MAGUFULI KUZINDUA BARABARA YA KIHISTORIA NCHINI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Mafuguli anatarajiwa kuizindua rasmi barabara ya juu ya Tazara leo hii . Barabara hiyo ni ya kwanza ya juu katika historia ya Tanzania , inayounganisha maeneo muhimu ya kiuchumi katika jiji la Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege wa Julius Nyerere, Bandari na hata barabara inayoelekea Viwandani.
Read MoreUzinduzi wa Flyover Tazara:
Viongozi mbalimbali wa Serikali na kichama wamewasili katika eneo la Tazara jijini Dar es salaam ambapo Leo inafanyika shughuli ya uzinduzi wa barabara ya juu. FlyOver Tazara. Katika hafla hiyo mgeni rasmi ni Mh Raisi Dr John Magufuli.
Read MoreKipigo cha aina hii ni Mara ya kwanza tangu 2015 La Liga.
Kwa mara ya kwanza tangu January 2015 Vigogo wa Soka Nchini Spain Barcelona na Real Madrid wanafungwa wote katika siku moja kwa vichapo toka kwa Sevilla na Leganes siku ya Jumatano. Mabingwa na vinara wa LA Liga wakajikuta wanachapwa 2-1 pale Butarque kwa Goli la mchezaji wa mkopo toka Madrid Oscar Rodriguez aliyeifungia Leganes goli la ushindi Baada ya makosa ya Beki Gerard Pique. Madrid nao wakawa na nafasi ya kukwea kileleni lakini kichapo makini cha goli 3-0 toka kwa Sevilla kikakwamisha ndoto za Kocha Julen Lopetegue. Baada ya mzunguko…
Read More