Watu kadhaa wametekwa nyara katika mashambulizi dhidi ya makanisa nchini Nigeria

Polisi wa Jimbo la Kaduna walmesema kwamba watu wenye silaha za kisasa walishambulia makanisa hayo mawili huko Kurmin Wali, jamii ya msitu katika wilaya ya Afogo, siku ya Jumapili yapata saa 5:25 mchana. Wachunguzi bado wanafanya kazi ili kuthibitisha idadi kamili ya watu waliotekwa nyara.

Msemaji wa polisi alielezea kwamba eneo hilo, lililotengwa na gumu kufikiwa kutokana na hali mbaya ya barabara, hufanya iwe vigumu kupata taarifa za kuaminika mara baada ya mashambulizi hayo.

Mchungaji John Hayab, kiongozi wa Chama cha Wakristo cha Nigeria kaskazini mwa nchi, ameliambia shirika la habari al Reuters kwa simu kwamba waumini 172 walitekwa nyara na kwamba tisa walifanikiwa kutoroka, na kuwaacha watu 163 bado wakishikiliwa mateka. "Viongozi wa kanisa wameniarifu kwamba waumini 172 wametekwa nyara, huku tisa wakifanikiwa kutoroka," Hayab amesema.

Nchini Nigeria, takwimu za awali mara nyingi hutofautiana sana baada ya utekaji nyara wa watu wengi. Idara za usalama kwa ujumla huwa zinapunguza idadi ya waathiriwa, huku jamii za wenyeji na makundi ya kidini wakati mwingine yakiripoti idadi kubwa zaidi. Hali kama hiyo ilitokea wakati wa utekaji nyara katika shule ya Kikatoliki katika Jimbo la Kaduna katika tukio lililopita.

Polisi imesema wanajeshi na vikosi vingine vya usalama vimetumwa katika eneo hilo na kwamba juhudi zinaendelea kuwatafuta watekaji nyara na kuwaachilia mateka.

Kaskazini Magharibi mwa Nigeria kumeshuhudia ongezeko la utekaji nyara wa watu wengi unaofanywa na magenge yenye silaha yanayoendesha harakati zao kutoka maeneo ya misitu, kushambulia vijiji, shule na sehemu za ibada.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii