Serikali imewaonya wananchi wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kudhalilisha viongozi au kusambaza taarifa za uchochezi na ikisisitiza kuwa haitawafumbia macho wanaokiuka sheria za matumizi sahihi ya majukwaa ya kidijitali.
Onyo hilo limetolewa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Angellah Kairuki wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari mkoani Dodoma, alipokuwa akitoa taarifa kwa umma kuhusu utekelezaji wa ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ndani ya siku 100 za uongozi wake.
Mhe. Kairuki amesema mitandao ya kijamii ni chombo muhimu cha mawasiliano na maendeleo, lakini matumizi yake lazima yawe na tija, heshima na kuzingatia sheria za nchi.
Ameeleza kuwa Serikali itaendelea kusimamia matumizi sahihi ya mitandao hiyo ili kulinda amani, mshikamano wa Taifa na heshima ya viongozi pamoja na wananchi kwa ujumla.
Aidha Waziri Kairuki amewahimiza wananchi kuitumia mitandao kwa kujenga jamii, kutoa taarifa sahihi na kuchochea maendeleo badala ya kusambaza maneno ya chuki na uchochezi.
Kwa taarifa zaidi tufuatilie na usikilize jembe Habari Kamili hapo saa saba kamili mchana ambapo msomaji wetu wa hii leo ni Jacob Mlay tafadhali usipitwe na taarifa zetu Mahiri kabisa.
Lakini pia tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Jembefmtz
#10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime