VIDEO YA DANSI YAUZWA KWA DOLA MILIONI MOJA

Video maarufu ya dansi ya mazishi ya wabeba jeneza wa Ghana ‘Coffin Dance’ imeripotiwa kupigwa mnada na kuuzwa kama mali ya kidigitali kwa dola milioni moja.
Nusu ya mapato ya video hiyo ambayo ilisambaa kwa kasi mitandaoni wakati wa janga la Covid-19 yataenda kwenye mashirika ya kutoa misaada ya Kiukreni wakati wa vita.
Video hiyo ilisambaa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2017 baada ya kuangazia nyimbo na dansi zao wakati wa kubeba masanduku ya miili katika ibada ya mwisho ya mazishi.
Na mwaka 2020, ilipata umaarufu zaidi baada ya watumiaji wa mitandao ya kijamii kuchukua dansi za kikundi hicho kuleta mzaha wakati wa janga hilo.
Video hiyo imeuzwa kwa kampuni ya kurekodi muziki ya Dubai ya 3FMusic Aprili 9, 2022.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii