Aneera Kabeer: Mwanamke wa Kihindi aliyebadili jinsia ambaye ombi lake la kutaka kufa limezua taharuki

Mnamo Novemba mwaka jana, Aneera Kabeer alihudhuria mahojiano yake ya 14 ya kutafuta kazi katika miezi miwili akiwa amevalia kofia, barakoa iliyoficha sehemu kubwa ya uso wake, na nguo za kiume.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 35, anasema kilikuwa kitendo cha kukata tamaa kutokana na matamshi ya kuchukiza aliyokumbana nayo kwenye mahojiano ya awali.

Alipata kazi ya muda - katika shule ya serikali katika jimbo la kusini mwa India la Kerala - lakini anadai alifukuzwa kazi isivyo halali chini ya miezi miwili baadaye.

Mkuu wa shule hiyo alikataa kutoa maoni yake. P Krishnan, afisa wa wilaya, alisema kwamba mkuu wa shule alimweleza kwamba Bi Kabeer hakufukuzwa kazi na badala yake, "hakuelewa hali hiyo".

Kutokana na chaguzi, Bi Kabeer aliwasiliana na huduma za usaidizi wa kisheria za serikali mwezi Januari - alitaka wakili awasilishe maombi ya euthanasia, au "mauaji ya huruma", kwa niaba yake.

"Nilichotaka ni kufanya kazi na kupata riziki. Lakini ikawa vigumu hata kufanya hivyo," Bi Kabeer asema.

Alikuwa amesoma kuhusu nchi ambazo ziliruhusu euthanasia na India iliruhusu tu euthanasia isiyo kamili.

"Nilijua singepata kibali cha kisheria hapa, lakini nilitaka kutuma ujumbe," anasema.

Badala yake, alitaka kupata usikivu wa serikali - na alifanya hivyo. Serikali ilijibu upesi, na sasa ana kazi nyingine.

Bi Kabeer anaonyesha wazi kwamba hakuwa na nia ya kujitoa uhai, na alichofanya hakikusudiwa kuwa mfano kwa wengine.

Lakini aina kama hizi za maandamano sio kawaida nchini India.

Kwa miaka mingi Wahindi wanaotafuta haki au mabadiliko ya kimfumo wamegoma kula, wamesimama kwenye maji hadi kiunoni kwa siku nyingi na kushikilia panya hai midomoni mwao.


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii