Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuandaa semina ya siku moja kwa wabunge wote ili kuwaelimisha juu ya athari za ongezeko la watu na mifugo, pamoja na shughuli nyingine za binadamu katika hifadhi ya Ngorongoro.
"Ni kweli upo mgongano mkubwa unaotokana na sheria tulizo nazo lakini pia matakwa binafsi ya mtu mmoja moja,lakin pia Mhe.Rais ametoa maelekezo ya kukutana na ndugu zetu waliopo pale na kazi hiyo tumeishaianza juma pili iliyopita nilianza kwa kukutana na viongozi wa Arusha nimewasikiliza,nimekutana na wizara pale Arusha nimewasikiliza hatua iliyobaki ni kwenda ngorongoro nitafanya mikutano na wananchi wa eneo hilo."alisema Mhe Kasimu Majaliwa.