ENOCK BELLA : "Wengi Hawakutaka Niwe Karibu na Mbosso"

Msanii wa Bongo Fleva Enock Bella yuko nchini Kenya kwa shughuli za kimuziki kuhakikisha anaongeza wigo mkubwa katika soko la muziki wake hususan mashabiki wapya ambao wanatakiwa kuwa nguzo muhimu katika jambo lake.

Sasa akiwa nchini humo, Enock Bella ameweka wazi kuhusu kile kilichokuwa kinaendelea baina yake na msanii mwenzake Mbosso kuhusu wao kutokuwa na maelewano mazuri kutokana na tuhuma za Bella kuwa Mbosso alikataa kumsaidia kimuziki.

Katika mahojiano na moja ya kituo cha Redio nchini humo weekend iliyopita, Enock Bella amesema kuwa kuna baadhi ya watu wao wa karibu ambao hawakupenda ukaribu wake na Mbosso hasa katika changamoto zao, jambo ambalo lilifanya suala hilo kuwa kubwa zaidi hasa kwa kumfanya mwenzake awe na hasira zaidi kwake.

“Kuna baadhi ya watu wetu wa karibu ambao walikuwa hawataki kabisa mimi kuwa karibu na Mbosso kutokana na mahojiano yale niliyayafanya na kumzungumzia. Waliamua kutumia nafasi hiyo kutuvuruga zaidi wakiamini wananiteketeza zaidi kimuziki lakini haijawa hivyo” alisema Enock Bella

Pia katika kukazia zaidi, watu hao anawafahamu vizuri na kama wataendelea kumchonganisha yeye na Mbosso, itafikia muda atawataja majina hadharani bila kuhofia chochote

Hata hivyo, Enock Bella alimuomba radhi Mbosso hadharani (kupitia mtandao wa Instagram) na Mbosso aliridhia bila kinyongo, hali ambayo inatafsiri kuwa wawili hao wamemaliza tofauti zao

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii