MOCCO GENIUS : "Mnanipa Ufalme Wangu au Niuchukue Kwa Lazima?"

Msanii na Mtayarishaji wa Muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania (Bongo Fleva), Mocco Genius amewauliza wadau na mashabiki wa muziki huo kuwa watampatia “Ufalme” wake kwa hiari, au auchukue kwa lazima?

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mocco Genius amesema kuwa yeye ndiye aliyetambulisha style ya Kompa nchini hasa kupitia nyimba mbali mbali kama vile MI NAWE (Feat. Marioo), MCHUCHU (Feat. Ali Kiba), FITINGI (Feat. Marioo) na nyinginezo kadhaa, sasa hivi wasanii wengi wanaufanya.

Hivyo akaamua kuhoji kama wadau wako tayari kumpatia Ufalme wake au auchukue kwa Lazima.

Wewe unashauri nini?

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii