Afungua Mashitaka Dhidi ya Wanandoa kwa Kutozwa Pesa ya Maji Harusini"

Mwanamke mmoja nchini Marekani ameamua kufungua mashitaka dhidi ya wanandoa wawili na waandaaji wa harusi aliyohudhuria kuwa kutokuifurahia harusi hiyo na utaratibu wote kiujumla.

Kupitia mtandao wa REDDIT, mwanamke huyo ambaye hakujitambulisha jina lake amesema kuwa amefikia hatua hiyo baada ya kutokuifurahia sherehe hiyo iliyokuwa imejawa na mapungufu mengi tofauti na vile ambavyo ilitarajiwa hasa kupitia kile kilichokuwa kimeainishwa katika taarifa za mwaliko

Katika maelezo yake ni kwamba, Sherehe hiyo ilifanyika katika eneo la uwazi yaani “outdoor” tofauti na ilivyoelezwa katika mwaliko, na kulikuwa na hali ya joto kali kutokana na jua kali. Pia ameongeza kuwa kelele za watoto wadogo takribani 8 zilikuwa ni kero kubwa sana wakati wa shughuli hiyo huku wazazi na waandaaji wakishindwa kuchukua hatua yoyote na kusababisa usumbufu kwake na waalikwa wengine

Mwanamke huyo hakuishia hapo, pia amelalamikia kitendo cha Bibi harusi na kaka yake kuanzisha vurugu za mara kwa mara kwa bwana harusi, hali ambayo ilifanya ratiba kusimama mara kwa mara na kusababisha usumbufu mkubwa.

Aidha kilichomkera zaidi, ni chakula cha waalikwa kuwa na wadudu aina ya Inzi hali iliyomfanya asifurahie chakula hicho na kupelekea kupata matatizo ya Tumbo. Na katika kuongezea juu ya hilo, Bibie huyo anadai kuwa alitozwa kiasi cha USD 2 (Tshs 5,130) pale alipoenda upande wa Bar ilyokuwepo eneo ili kujipatia maji ya kunywa kutokana na joto kuwa kali sana

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii