Aliyedai kuwa ni Mtoto wa Jay Z afuta Mashitaka

SAKATA la Rapa Jay Z na Kijana anayedai kuwa ni Mtoto wake halali hatimaye limefikia ukumbini baada ya Kijana huyo kuiomba mahakama kufutilia mbali mashitaka hayo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Kijana Rymir Satterthwaite (30) alichapisha kipande cha video kikimuonesha kuthibitisha kuwa ameamua kuachana na Kesi aliyoifungua dhidi ya Jay Z kuwa ni baba yake mzazi na amemtelekeza kwa kipindi cha muda mrefu tangu alipomuacha mama yake akiwa mjamzito.

Rymir ameongeza kuwa, kuachana na kesi hiyo sio kwamba ameshindwa kuendelea nayo, bali ni maamuzi yake na utashi wake binafsi ambavyo vimemsukuma kufikia hatua hiyo, ili aweze kuendelea na maisha mengine kama ambavyo ilikuwa hapo awali.

Ikumbukwe kuwa, Kijana huyo ilijitokeza miaka kadhaa iliyopita akisema kuwa yeye ni mtoto halali wa Jay Z ambaye alikuwa na mahusiano na mama yake (Rymir) miaka ya 1990 , hivyo anahitaji haki yake ya msingi kimalezi kutoka kwa baba yake.

Hata hivyo, Jay Z alijitokeza hadharani na kukana kauli ya kijana huyo, huku akiitaka mahakama kuitupilia mbali kesi hiyo, kwa sababu hata vipimo vya DNA havikuthibitisha kama Rymir ni mtoto wake kibaiolojia.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii