Katy Perry Kwenye Penzi Jipya na Waziri Mkuu Mstaafu

MSANII wa Muziki wa Popnchini Marekani, Katty Perry, hatimaye “amezama” katika penzi jipya na Waziri Mkuu mstaafu wa Canada, Justin Trudeau zikiwa zimepita wiki chache tangu ithibitishwe kuwa  ameachana na aliyekuwa mchumba wake Orlando Bloom.

Perry (40) na Trudeau (50) walinaswa na Kamera za mmoja wa mashabiki wa muziki wake katika mgahawa maarufu nchini Canada, unafahamika kwa jina la Le Violon, na wawili hao walikuwa katika mazungumzo yenye furaha nzito huku yakitawaliwa na chembechembe za mahaba mazito ndani yake.




Ingawa wawili hao hawajathibitisha rasmi kuhusu uhusiano huo, lakini viashiria vyote vilivyoonekana katika Mgahawa huo, vilijenga taswira ya kuwepo kwa mahusiano baina ya wawili hao.

Trudeau aliachana na Mke wake Sophie Gregoire Trudeau mwaka 2023 baada ya kudumu katika ndoa kwa muda wa miaka 18 wakifanikiwa kupata watoto watatu, na mnamo mwezi Januari mwaka huu, aliamua kujiuzuru nafasi ya Waziri Mkuu nchini Canada kutokana na masuala mbali mbali ya kiuongozi.

Kwa Upande wa Katty Perry yeye amefanikiwa kupata mtoto mmoja na aliyekuwa Mchumba wake, Orlando Bloom

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii