Ombi La Baba Levo Baada ya "Kutoboa" Sita Bora

MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Baba Levo ametoa ombi lake kubwa kwa wasanii mbali mbali hapa nchini baada ya jina lake kupitishwa kati ya wagombea  Sita watakaopitia mchujo wa pili wa kuipeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye nafasi ya Ubunge Kigoma Mjini.

Katika Melezo yake, Baba Levo amewaomba wasanii hao ambao wanamuunga mkono kwa moyo mmoja, kurekodi vipande vya Video wakimuombea Kura kwa wajumbe ambao ndio wana jukumu la kukamilisha mchakato unaofuata.

Baba Levo alitajwa kuwa miongoni mwa watia nia wengine (6 Bora) ambao sasa Wajumbe ndo watakaoamua nani mwenye sifa za kupiga hatua Zaidi.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii