UTAFITI: Ishara Ya Jicho Inaweza Kukusaidia Haraka Zaidi.

Watafiti kutoka chuo kikuu cha Flinders kilichopo nchini Australia, wamesema kuwa mawasiliano ya ishara kwa njia ya jicho, ndiyo njia sahihi Zaidi inayoweza kukupatia kile unachohitaji ndani ya muda huo kwa haraka Zaidi.

Inafahamika kuwa mara nyingi Jicho/Macho hutumika kuwasiliana kwa njia ya siri kati ya watu wawili au Zaidi, lakini ndiyo lugha ya ishara ambayo mara nyingi urahisi wake katika kufikisha ujumbe huwa ni mkubwa Zaidi ndani ya muda mfupi

Dr. Nathan Caruana ambaye ni Mkufunzi na Mtafiti katika chuo hicho, amesema kuwa wamefanikiwa kufanya utafiti kwa watu Zaidi ya 137 kwa kuwahoji maswali mbali mbali kwa nadharia na vitendo, kisha kubaini kuwa siri kubwa iliyojificha katika ishara kwa njia ya jicho/macho ni kwamba inarahisisha zaidi mawasiliano.

Aidha Dr. Caruoana ameongeza kuwa, iwapo itatokea mtu akahitaji msaada wa kitu flani ambacho kipo mbali na anahitaji aliye karibu nacho ampatie, basi akimtizama na kukitizama kitu hicho kwa wakati mmoja, ni rahisi sana kukipata tofauti na vinginevyo.

“Hata ikatokea una hisia na mtu, ukimkonyeza tu ataelewa hitaji lako. Achilia mbali suala hilo, umakini wa kumtazama mtu wakati anaongea, huashiria anachokisema unakielewa. Pia kama mtu amekosea, unaweza kumwambia kwa siri kupitia jicho lako na akajirekebisha” alisema Mtafiti huyo

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii