FAT JOE : BIFU LANGU NA 50 CENT PAMOJA NA JAY Z LILININYIMA MABILIONI YA PESA"

Rapa Fat Joe amesema kuwa “Bifu” lake kubwa dhidi ya 50 Cents na Jay Z lililotokea katika miaka ya 2000, lilimgharimu mabilioni ya fedha kitu ambacho hatokuja kukisahau katika maisha yake.

Akizungumza kupitia Podcast ya “Sneaker Shopping”, Fat Joe ambaye alikuwa ni kiongozi wa TERROR SQUARD amesema kuwa, ugomvi huo baina yake na wasanii hao wawili uliovuma kweli kweli, ulimfanya apoteze “Dili” la mabilioni ya fedha alilokuwa amelipata kupitia chapa za AIR JORDAN na REEBOK.

Katika maelezo yake, mkali huyo wa wa “Make It Rain” amefafanua kuwa, Michael Jordan aliamua kusitisha kabisa dili lake na Fat Joe (Air Jordan) baada ya kutokea sintofahamu na mvutano mkubwa baina yake (Fat Joe) dhidi ya 50 Cents katika tuzo za MTV VMA’s zilizofanyika mwaka 2005.

“Michael Jordan aliniita akaniambia, Fat Joe, mimi sio mtu wa migogoro na ugomvi. Jambo letu tulitazame kipindi kijacho” alisema Fat Joe

Pia alimalizia kwa Kusema kuwa, Kampuni ya Reebok iliahidi kupiga naye biashara ya mabilioni ya fedha, lakini ilipogundua kuwa alikuwa na ugomvi na Jay Z, haraka sana walisitisha dili hilo na kuyeyuka kwa staili hiyo

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii