Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza ushuru mpya kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka nje, ikiwemo dawa na malori.
Ametangaza kuongeza ushuru hadi asilimia 100 kwa dawa zinazotengenezwa nje kwa kutumia leseni za kampuni za Kimarekani, au zile zinazozalishwa ndani ya Marekani lakini kuuzwa kwa majina tofauti.
Hatua hii itaanza kutekelezwa kuanzia Oktoba 1, isipokuwa kwa kampuni zitakazojenga viwanda vya uzalishaji ndani ya Marekani.
Aidha, serikali ya Marekani imeweka ushuru wa asilimia 25 kwa malori makubwa ya kubeba mizigo, huku ushuru kwa vifaa vya jikoni na vya bafuni ukiongezwa kwa asilimia 50.
Rais Trump amesema kuwa hatua hiyo inalenga kulinda masoko ya ndani.