CARDI B: "Wasanii Wa Kike Niliowasaidia Waliishia kunisaliti mpaka Kuchepuka Na Mwanaume Wangu"

Msanii wa Kike katika soko la Rap, Cardi B amefunguka kuwa wasanii wengi wa kike aliowasaidia walimgeuka, wakamsaliti mpaka kufikika hatua ya “Kuchepuka” na Mume wake.

Akipiga stori na msanii mwenzake Kelly Rowland, Cardi B lisema kuwa ni wasanii wengi sana wa kike ambao amewasaidia katika soko la muziki na kupata mafanikio makubwa, lakini mwisho wa siku alichoambulia ni kusalitiwa mpaka kufikia hatua ya kumsaliti na mume wake (Japo hajataja ni nani).

Katika maelezo yake, Cardi ameongeza kuwa, ilifikia hatua alikuwa akiwafuata wasanii hao katika DM zao ili kuwahamasisha wapambane na kuwatia moyo Zaidi, ila mwisho wake aliambulia maumivu ya moyo.

“Nilichokuja kugundua na kujifunza, ni kuwa unakuwa mwema kwa mtu wa aina gani” alisema Cardi B

Rappa huyo wa kike ambaye pia ni mshindi wa tuzo za Grammy, ametangaza kuachia Album yake mpya aliyoipa jina la “AM I THE DRAMA?” na itaingia rasmi sokoni SEPTEMBA 19, 2025

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii