Pakistan yafanya maandalizi ya mazungumzo ya amani

Pakistan imeendeleza leo maandalizi ya duru mpya ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran siku chache kabla ya makubaliano ya kusitisha mapigano kukamilika.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema wapatanishi wa Marekani wataelekea Pakistani leo, lakini haijabainika wazi kama mipango hiyo itabadilika.

Kwa upande wake, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran Esmail Baghaei, amewaambia waandishi wa habari mjini Tehran leo kwamba hakuna maamuzi yaliofikiwa kuhusu mazungumzo hayo.

"Kwa sasa, nikiwa nahudumu, hatuna mipango ya awamu inayofuata ya mazungumzo, na hakuna uamuzi wowote uliotolewa kuhusu hili."

Huku hayo yakijiri, China imeelezea leo wasiwasi kuhusu hatua ya  Marekani ya kukamata meli yenye bendera ya Iran iliyojaribu kukwepa kizuizi cha majini, na kuzitaka pande zote mbili kurejelea mazungumzo ya amani. 

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii