Upinzani nchini DRC unajaribu kuungana dhidi ya marekebisho ya katiba. Mnamo Mei 6, 2026, wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Rais Félix Tshisekedi alifungua mlango wa muhula wa tatu unaowezekana kufuatia kura ya maoni ya kikatiba.
Msimamo huu ulishutumiwa na vyama kadhaa vya siasa vya upinzani ndani ya nchi na uhamishoni. Jukwaa hilo, linaloitwa C64 (Muungano wa Kifungu cha 64, kifungu cha kikatiba kinachosimamia haki ya upinzani wa raia), lilizinduliwa siku ya Jumanne, Mei 19, katikati mwa jiji la Kinshasa.
Saa sita mchana, Kituo cha Boboto mjini Kinshasa kilikuwa kimejaa watu. Wanaharakati walikuwepo. Chumba kilikuwa kimejaa watu, na kila mtu alikuwa akisubiri viongozi wakuu wa upinzani kutoa tangazo. Jukwaa hili litajumuisha sehemu kubwa ya upinzani: Lamuka inayoongozwa na Martin Fayulu, Muungano wa Kushoto ukiongozwa na Jean-Marc Kabund, Ensemble ikiongozwa na Moïse Katumbi, Envol ikiongozwa na Delly Sessanga, na hatimaye LGD ikiongozwa na Matata Ponyo. "Pia kuna zaidi ya vyama vya kiraia 50 vilivyojiunga kutekeleza "kutekeleza harakati za kiraia ," anaongeza Prince Epenge wa Lamuka.
Hakuna wafuasi wa Kabila, na hakuna uwakilishi wa Rais wa zamani Joseph Kabila. "Mstari wetu mwekundu," anaelezea mshirika wa karibu wa Martin Fayulu, "ni kuunga mkono M23." Kwa hivyo, pia hakuna mwakilishi wa muungano wa "Sauvons la RDC ", ambao ulizinduliwa miezi michache iliyopita karibu na Rais wa zamani Joseph Kabila. Mmoja wa wanasiasa ametuambia kwamba Matata Ponyo ameachana na uongozi wa Sauvons DRC na kujiunga na C64.
"Vita vimeanza." Tangazo hili kutoka kwa upinzani lilitarajiwa kwa siku kadhaa. Inajulikana kwamba baada ya mkutano wa waandishi wa habari na rais Félix Tshisekedi wa Mei 6, ambapo alijadili waziwazi uwezekano wa muhula wa tatu, upinzani ulikusanya vikosi vyake na kupanga uhamasishaji kuzunguka mpango wa utekelezaji wa pamoja.
Umoja huu haukufikiwa bila matatizo: "Tulitambua kinachotuunganisha na kutugawanya," anaelezea Prince Epenge, "lakini hatimaye, kinachotuunganisha ndicho muhimu zaidi." Lengo: kuzuia marekebisho au mabadiliko yoyote kwenye Katiba, haswa kifungu kinachoweka kikomo cha muhula. "Kifungu cha 220 cha Katiba ni Mlango-Bahari wetu wa Hormuz. Hatutagusa," anasisitiza Prince Epenge.
Mpango wa utekelezaji bado haujafichuliwa, lakini "vita vimeanza," anaonya mwansiasa huyu wa C64. "Leo ilikuwa uzinduzi rasmi wa muungano; hatukutaka kuchanganya mambo," anaelezea Emery Okundji, Katibu Mkuu wa FONUS. "Hivi karibuni, kutakuwa na ratiba inayoelezea hatua maalum tutakayochukua."
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime