Mashabiki wa msanii wa Afrika Kusini, Tyla, wameibua taharuki mtandaoni baada ya nyota huyo kuzima akaunti zake za X na TikTok huku akiifanya akaunti yake ya Instagram kuwa ya faragha kuelekea kuachia albamu yake mpya inayotarajiwa kujulikana kama APop*.
Hatua hiyo imewaacha mashabiki wengi wakiwa na maswali mengi, hasa kutokana na muda ambao umeonekana kuwa wa muhimu katika kampeni ya kuitangaza albamu hiyo ya pili ya Tyla. Wafuasi waliokuwa tayari wanamfuatilia kwenye Instagram bado wanaweza kuona machapisho yake, lakini watumiaji wapya sasa wanatakiwa kutuma maombi ya kumfuata kabla ya kuona maudhui yake.
Baadhi ya mashabiki wameeleza kuwa huenda Tyla ameamua kupumzika kutoka kwenye mitandao ya kijamii kutokana na maneno makali na ukosoaji anaokumbana nao mara kwa mara mtandaoni, huku wengine wakiamini hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa kutangaza albamu yake mpya.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime