Achraf Hakimi kushtakiwa rasmi kwa ubakaji

Mahakama ya Rufaa nchini Ufaransa imethibitisha leo kuwa nyota wa soka wa Morocco, Achraf Hakimi, atashtakiwa rasmi na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumbaka mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 24.

Mnamo Februari 2023, mwanamke huyo aliwasilisha ripoti kwa polisi katika eneo la Val-de-Marne, kusini mashariki mwa Paris, kwamba Hakimi alimbaka.

Hakimi, ambaye anachezea klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) na pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Morocco, amekuwa akikanusha tuhuma hizo tangu zilipoibuka.

Taarifa hii inakuja wakati timu ya Morocco ikijiandaa kucheza mechi yake ya pili ya Kombe la Dunia dhidi ya Scotland baadaye hii leo.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii