Anavyogeuza taka kuwa mboleahai
IKIWA kuna msemo unaomfafanua vyema Richard Mwangi, basi ni huu: “Nipe tatizo, nitaligeuza kuwa fursa yenye thamani.”
Mwangi ndiye mwanzilishi na Afisa Mkuu Mtendaji wa Organic Fields Ltd, kampuni inayojishughulisha na uundaji wa mboleahai kutokana na taka za chakula.
Kampuni hiyo iko katika eneo tulivu la Kwihota, Ruiru, Kaunti ya Kiambu, ambako taka za chakula hugeuzwa kuwa bidhaa muhimu kwa wakulima – mboleahai.
Safari yake imetokana na msingi wa tajiriba na malengo, ambapo baada ya kufanya kazi na wakulima, hasa wadogo, kwa zaidi ya miaka 10, Mwangi alishuhudia changamoto zao.
Ingawa serikali inaendelea kuweka mikakati kukabiliana na baa la njaa na kuhakikisha usalama wa chakula, mjasiriamali huyu anaamini kuwa suluhisho linaanzia kwa kuboresha mbinu za kilimo.
Isitoshe, anaona Kenya kuendelea kuagiza kutoka nje mbolea – hasa fatalaiza ambazo kwa kiwango fulani zimesheheni kemikali ndiyo changamoto kuu inayopaswa kuangaziwa.
“Kwa zaidi ya miaka kumi – muda ambao nilihudumia wakulima, niligundua afya ya udongo na mbinu bora za kilimo ndizo msingi wa kuongeza kiwango cha uzalishaji chakula,” Mwangi anasema.
Ni gapu hiyo na kuendelea kuharibiwa kwa udongo na vilevile mazingira kulimchochea kuasisi Organic Fields Ltd mwaka wa 2016.
Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii