Umoja wa Ulaya kulisaidia jeshi la DRC kuboresha oparesheni zake

Umoja wa Ulaya  katika taarifa kwa vyombo vya habari  mapema wiki hii ulitangaza kutoa  karibia Euro Milioni 10 kwa  FARDC kabla ya mwisho wa mwaka ujao kuboresha operesheni ya jeshi la DRC

Ufadhili huo utakwenda moja kwa moja kwa   jeshi la Kongo  kulisaidia kupata vifaa ili kuimarisha uwezo wake wa kufanya kazi. Vifaa hivi vitajumuisha zana za mawasiliano,kuboresha operesheni, vifaa vya matibabu pamoja na  vifaa vya kuwezesha  jeshi hilo kushika doria  kwenye mipaka  na  mito.

Uwasilishaji wa kwanza umepangwa kufanyika ya kabla ya mwisho wa 2026.

Hii ni awamu ya  pili ya ufadhili kutolewa kwa FARDC kutoka  Umoja wa Ulaya.

Awamu ya kwanza, iliyotolewa  mwaka wa 2023, ililenga kusaidia kikosi cha 31 kilichoko eneo la  Kindu.

Kutokana na msaada huu  sasa  jumla ya missada kutoka kwa mfumo wa amani wa Ulaya kwa FARDC umefikia Euro Milioni 30.

Msaada huu ni sehemu ya juhudi za Umoja wa Ulaya kuimarisha mageuzi ya sekta ya usalama nchini DRC na kuunga mkono FARDC katika oparesheni zake kulinda raia na kurejesha mamlaka ya serikali, huku ikichangia mchakato wa amani.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii