Simba Yakutana na Kaa la Moto

Pazia la NBC Premier League msimu wa 2026/27 linatarajiwa kufunguliwa rasmi Agosti 14, huku timu mbalimbali zikianza kampeni ya kusaka pointi tatu katika ratiba yenye michezo kadhaa ya kuvutia na yenye ushindani mkubwa.

Simba ni miongoni mwa timu zinazokabiliwa na ratiba ya moto katika michezo yake ya mwanzo, baada ya kumaliza msimu uliopita katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 73, nyuma ya mabingwa Yanga SC waliomaliza na pointi 75.

Mnyama atafungua kampeni yake Agosti 16 kwa mchezo dhidi ya Kagera Sugar, timu iliyopanda daraja kutoka Championship, katika Uwanja wa Kaitaba.

Baada ya hapo, Simba itakuwa ugenini tena Agosti 19 dhidi ya Pamba Jiji FC katika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, kabla ya Agosti 22 kukutana na Singida Black Stars katika Uwanja wa Airtel.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii