Mwaka mmoja bila Rais Magufuli

 

Machi 17, 2022, Tanzania inaadhimisha mwaka mmoja wa kifo cha rais wa awamu ya tano wa taifa hilo, John Magufuli.

Magufuli alifariki kutokana na matatizo ya moyo jijini Dar es Salaam.

Makamu wake wa rais wakati huo, Samia Suluhu Hassan, akarithi kiti chake kwa kuapishwa siku mbili tu baadaye yaani Machi 19, 2021 na kuwa Rais wa awamu ya sita na wa kwanza mwanamke katika historia ya taifa hilo la Afrika Mashariki.

UCHUMI KWENYE UTAWALA WA JPM


Uchumi wa Tanzania umekuwa ukikua kwa wastani wa asilimi 6.3 kati ya mwaka 2010 mpaka 2019 ikiwa miongoni mwa nchi chache barani Afrika ambazo uchumi wake unakua kwa kasi.

Licha ya kuendelea kuimarika kwa uchumi wake chini ya Rais Samia lakini hilo halitafsiri maisha halisi ya mtanzania, kama mtaalamu huyu wa fedha alivyoiambia BBC: "Ipo tofauti ya ukuaji wa uchumi na maendeleo na uchumi, sasa tunashuhudia angalau ahueni mifukoni ukilinganisha na kipindi cha Rais Magufuli kati ya mwaka 2018 na 2020, ingawa bado mambo magumu, maisha magumu', anasema Raphael Magoha.

MIMBA MASHULENI

Mmoja wa wazazi wa binti ambaye alishindwa kuendelea na shule kwa sababu ya ujauzito, anasema atamkumbuka Rais Magufuli kwa jitihada zake za kukuza uchumi na kuboresha miundo mbinu, lakini sera yake ya mabinti wajawazito kutorudi shuleni lilimtatiza na kukata tamaa ya maisha ya kuchumi ya mwanae huko mbele.

'elimu ndio tegemeo letu sisi masikini, unaamini mtoto wako akisoma atajisaidia na atakuja kusaidia familia, kidogo azime ndoto za maelfu ya mabinti, tunashukuru mama (Rais Samia) kaliona hilo, mabinti wajawazito sasa wameruhusiwa kuendelea na masomo.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii