Mwili wa Papa Francis umepelekwa Kanisani, huku maombolezo yakiendelea.
Akiwa hai, Papa Francis aliomba kuzikwa katika Kanisa la Mtakatifu Maria Major Basilica na sio Mtakatifu Petro, eneo ambalo viongozi wa Kanisa hilo huzikwa. Watu wanatarajiwa kuanza kumuaga siku ya Jumatano.
Kote duniani, baada ya kifo chake, Wakiristo na wasio Wakiristo wamekuwa wakifurika katika Makanisani, kuhudhuria misa ya kumkumbuka kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki.