UGANDA YAVUNJA USHIRIKIANO WA KIJESHI UJERUMANI

 Jeshi la Uganda limesema nchi hiyo imesimamisha ushirikiano wote wa kijeshi na Ujerumani huku likidai kuwa balozi wa Ujerumani anajihusisha na shughuli za uasi katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.


Hapo awali jeshi la nchi hiyo lilishutumu baadhi ya balozi za Ulaya kwa kuyaunga mkono makundi ya uasi na wasaliti huku likimutenga balozi wa Ujerumani Matthias Schauer.

Kufuatia ripoti yakwamba wanadiplomasia kuikosoa tabia ya mtoto wa Rais Yoweri Museveni Muhoozi Kainerugaba ambaye ni mkuu wa jeshi.

Kainerugaba ambaye anatajwa kuwa na uwezekano mkubwa wa kumrithi babake mwenye umri wa miaka 80 kama rais ambaye anajulikana kwa kuandika machapisho yake yenye utata kwenye mitandao ya kijamii.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii