Habari potofu zinazotumika kumtukuza kiongozi Ibrahim Traore

Moshi unapanda kutoka kwenye jengo huku Beyoncé, akiwa amevalia mavazi ya kivita, akipanda gari la kivita. Kapteni Ibrahim Traoré, kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso, yuko kwenye video ya muziki pia, na anafyatua bunduki. "Mungu amlinde Ibrahim Traoré katika vita kwa ajili ya njia ya watu, akivunja minyororo kutoka kwenye himaya," yanasema maneno ya wimbo huo.

Lakini si Beyoncé au Ibrahim Traoré. Video ni ya kina, aina ya maudhui yaliyoundwa kwa akili mnemba ili kuonekana halisi.

Mamia ya video zinazotolewa na AI zikimuonesha Bw Traoré kama shujaa wa Afrika nzima, nyingi zikiwa na taarifa za uongo, zimekuwa zikijaa kwenye mitandao ya kijamii kote Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara tangu mwishoni mwa Aprili.

Mwenendo huo ni mkubwa, huku watumiaji wa mitandao ya kijamii kwenye X, Facebook, Instagram, TikTok, WhatsApp, na Youtube kutoka nchi kama Nigeria, Ghana na Kenya, wakimsifu Bw Traoré kama mfano kwa viongozi wengine wa Afrika.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii