SHEIKH HASSAN KABEKE" KUWENI WAZALENDO"

Watanzania wametakiwa kuwa wazelendo ili kuilinda nchii  kuelekea kipindi  cha uchaguzi  unaotarajia kufanyika mwaka huu

Hayo yamesemwa na sheikh wa mkoa wa Mwanza Hasani Kabeke wakati akitoa hutuba ya swala ya ijumaa katika msikiti Mkuu wa bakwata mkoa wa Mwanza


Kabeke amesema ni jukumu la kila mtanzania kuhakikisha anakuwa  mzalendo kwa Nchii yake, kuwa makini haswa kipindi hiki Nchii inaelekea kwenye uchaguzi mkuu kutoanzisha migogoro ambayo inaweza leta mpasuko kwenye Taifa 


Aidha Kabeke amewataka wanasiasa kuwa wazalendo,kwa kufanya siasa safi zisiso za uchonganishi baina ya raia na viongozi wao huku akiwataka vijana kujikita kutafuta kipato,kuwa na maadili  na kuacha kutumika na wanasisa kuchafua Nchii yao.

IMEANDIKWA NA MUSTAFA KINKULAH

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii