ZITTO ZUBERI KABWE YUPO TAYARI KUELEZA UKWELI MAHAKAMANI

 Mei 18, 2025  jijini Dar es Salaam kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe, alisema amefunguliwa kesi mahakamani na Mfanyabiashara Harbinder Seth ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya (IPTL) akidai kuwa Zitto amemkashifu na kumvunjia heshima mbele ya jamii kupitia chapisho lake kwenye ukurasa wa X (zamani Twitter) kuhusu sakata la IPTL.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Zitto alisema kuwa licha ya Seth kudai fidia ya mabilioni ya fedha yeye haogopi na yupo tayari kwenda mahakamani kusimamia kile alichokiandika huku akisisitiza kuwa ni kweli na kinaakisi hali halisi ya sakata hilo.
Zitto alisema kuwa chapisho lake kwenye mtandao wa X lililolalamikiwa lilikuwa na nia njema ya kuleta ufumbuzi wa sakata la IPTL, na kwamba kama aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Hesabu za Serikali (PAC) aliyeshughulikia suala hilo, ana taarifa sahihi na za kweli alizotumia kuwafahamisha wananchi.
“Kesi hii itanipa nafasi ya kuweka ukweli wote hadharani na kuuzika kabisa mzoga huu uitwao sakata la IPTL. Maneno yale niliyoyaandika ni ya kweli, na ni wajibu wangu kama Mtanzania kulinda rasilimali za Taifa dhidi ya uporaji wa aina yoyote kwa kivuli cha uwekezaji,” ameongeza.
Zitto amehitimisha kwa kumwambia Harbinder Seth kuwa yuko tayari kukutana naye mahakamani na atatumia nafasi hiyo kueleza ukweli wote kuhusu sakata hilo.
Ili kupata taarifa zaidi endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya www.jembenijembe.com kupitia Instagram ,Facebook, tikok,x zamani twitter pamoja na YouTube 

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii