CHAUMMA WAPOKEA WANACHAMA WAPYA KUTOKA CHADEMA

Wajumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA iliyomaliza muda wake akiwemo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara Benson Kigaila, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu CHADEMA Zanzibar, Salum Mwalimu, Catherine Ruge na aliyekuwa Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano, John Mrema ambao walitangaza kujiondoa CHADEMA kuanzia May 07,2025 hatimaye wamehamia rasmi Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) wakiwa pamoja na wengine akiwemo Devotha Minja.


Mwenyekiti wa CHAUMMA, Mzee Hashim Rungwe amewapokea Wanachama hao wapya na kuwakabidhi kadi za CHAUMMA Jijini Dar es salaam leo May 19,2025 kwenye Mkutano Mkuu wa CHAUMMA.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii