Watu 31 Wauawa Shambulio la Israeli Lebanon

Takriban watu 31 wameuawa kufuatia shambulio la anga lililofanywa na Israel nchini Lebanon mapema leo, kwa mujibu wa mamlaka za Lebanon.

Mashambulizi hayo yanatajwa kuwa ni sehemu ya mvutano unaoendelea kati ya pande hizo mbili, uliokithiri baada ya kundi la wanamgambo la Hezbollah linaloungwa mkono na Tehran kurusha roketi kuelekea Israel ambapo hatua hiyo ilidaiwa kufuatia kuuawa kwa kiongozi mkuu wa Iran.

Jeshi la Israel limeapa kuongeza operesheni zake za kijeshi nchini Lebanon, likisema litalifanya kundi la Hezbollah kulipa “gharama kubwa” kwa mashambulizi yake.

Tayari Israel imetekeleza mashambulizi kadhaa katika vitongoji vya kusini mwa mji wa Beirut na maeneo ya kusini mwa Lebanon, ambako Hezbollah ina ushawishi mkubwa.

Hata hivyo mvutano huo unaendelea kuzua hofu ya kuongezeka kwa mapigano katika eneo la Mashariki ya Kati, huku juhudi za kidiplomasia zikitajwa kuhitajika ili kupunguza hali ya sintofahamu.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii