Ghana, Cote d'Ivoire kukutana mechi za kufuzu AFCON 2027

Ghana wamepangwa katika kundi moja na Cote d'Ivoire wakati draw ya mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika - AFCON 2027 ilipofanywa jana mjini Cairo.

Gambia na Somalia zinakamilisha Kundi C na vinara pamoja na watakaomaliza wa pili katika kundi baada ya mechi sita kati ya Septemba na Machi watafuzu kwa mashindano hayo maarufu ya CAF. Cote d'Ivoire, Ghana na Cape Verde ni miongoni mwa timu 10 za Afrika zilizofuzu kucheza Kombe la Dunia la 2026, litakaloanza mwezi ujao nchini Marekani, Kanada na Mexico.

Cape Verde, wako katika Kundi K la AFCON pamoja na Mali, Rwanda na Liberia. Afrika Kusini iko katika Kundi D na Guinea, wenyeji wenza Kenya na Eritrea. Kwa kuwa Wakenya watafuzu moja kwa moja, timu zingine tatu zitapigania tiketi moja ya kuelekea Afrika Mashariki.

Nigeria pia wako katika kundi ambalo kutakuwa na mechi moja tu ya kufuzu, mbali na wenyeji wenza Tanzania. Madagaska na Guinea-Bissau wanakamilisha Kundi L.

Mabingwa watetezi Morocco wako katika Kundi A pamoja na Gabon, Niger na Lesotho. Senegal, walioshika nafasi ya pili katika AFCON 2025, watakabiliana na Msumbiji, Sudan na Ethiopia katika Kundi J.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii