Upinzani wawataka wakazi wa mji wa Kinshasa kusalia majumbani mwao

Sehemu ya upinzani chini DRC, umewataka wakazi wa mji mkuu wa nchi hiyo, Kinshasa kusalia majumbani mwao. Mpango huu unaongozwa na vuguvugu la C64, ambalo linaundwa na vyama vya kisiasa kadhaa kupinga marekebisho ya katiba ambayo serikali ya sasa inataka, marekebisho ambayo yanaweza kumruhusu rais Felix Tshisekedi kusalia madarakani baada ya muhula wake wa pili kumalizika.

Siku hii ya "mgomo wa jumla" ni hatua ya kwanza kuchukuliwa na C64 na inaonekana kama kipimo cha uwezo wake wa kuhamasisha wafuasi wa upinzani.

"Kila mtu anambwa kusalia nyumbani": Hii ni kauli mbiu iliyochaguliwa na wale wanaopinga marekebisho ya katiba, kutoka jukwaa la C64. Kwa siku hii, hakuna maandamano au mikutano iliyopangwa, lakini ni kipimo cha uwezo wake wa kuhamasisha wafuasi wa upinzani. "Hatuna shaka, tunajua watu wanataka nini," viongozi kadhaa wa vuguvugu hilo wamesema.

Kwa upande mwingine, muungano tawala hauna imani sawa na hautarajii idadi kubwa ya watu kujitokeza. Kwa kweli, "hatujapanga maandamano ya kupinga mgomo wa upinzani," amesema mfuasi mmoja wa chama cha rais cha UDPS, "lakini tutakuwa macho kuhakikisha kwamba wakazi wa Kinshasa wanaweza kwenda kazini kama kawaida."

"Wajibu wa kwenda kazini"

Mamlaka ya DRC, kwa upande wake, imewataka mara kwa mara watumishi wa umma kwenda kazini. Waziri wa Utumishi wa Umma ametoa taarifa akiwakumbusha wafanyakazi kuhusu "kutoegemea upande wowote kisiasa kwa utawala" pamoja na "wajibu wa kwenda."

"Kufanikiwa au kushindwa kwa wito wa mgomo wa jumla kunategemea saa chache za kwanza za siku," anasema mwanasiasa mmoja, akiongeza: "Kiashiria pekee cha kuaminika cha uhamasishaji unaowezekana kitakuwa uwepo au kutokuwepo kwa msongamano wa magari."

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii