WHO yapunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya wagonjwa wanaoshukiwa nchini DRC na Uganda

Marekebisho haya ya takwimu hayamaanishi kwamba mlipuko wa virusi vya Ebola umepungua. Ni matokeo tu ya uelewa bora wa hali ya mlipuko huo, kutokana na kuwasili kwa vipimo na vitendanishi 2,000 huko Bunia wiki iliyopita.

Shirika la Afya Duniani (WHO) lilirekebisha kwa kiasi kikubwa makadirio yake ya idadi ya wagonjwa wanaoshukiwa kuambukizwa virusi vya Ebola Bundibugyo nchini DRC na Uganda siku ya Jumanne, Juni 2. Idadi hiyo ilishuka kutoka 906 hadi 116, kwa wagonjwa 330 waliothibitishwa, ikiwa ni pamoja na wagonjwa 321 nchini DRC.

Marekebisho haya ya takwimu ni matokeo ya kuwasili Bunia wiki iliyopita kwa vipimo na vitendanishi 2000 ambavyo viliwezesha kushughuliki sampuli zote zinazosubiri uchambuzi na hivyo kuondoa maambukizi ya virusi kwa wagonjwa wengi ambao walikuwa wakiugua magonjwa mengine.

Pia inaonyesha jinsi vipimo vinavyosalia muhimu katika kukabiliana na ugonjwa huu hatari, kwani ni muhimu kwa kupata uwazi kuhusu kiwango halisi cha maambukizi na vifo vinavyosababishwa na virusi vya Ebola, na pia kwa ajili ya kuorodhesha visa vilivyorekodiwa. Hata hivyo, vipimo hivi bado havitoshi nchini DRC, ambapo vinasaliai kuwa na mahitaji makubwa.

Vikwazo kadhaa vinavyozuia uelewa sahihi wa hali ya mlipuko

Siku ya Jumatatu, Juni 1, maabara ya Bunia, kwa mfano, ilipokea sampuli 65 lakini iliweza kupima 18 pekee. Kati ya hizi, 12 zilipimwa na kupatikana na virusi. Tatizo la uwezo huu wa kutosha wa kupima sampuli zilizopo ni kwamba zinachelewesha uthibitisho wa utambuzi na kuanza kwa matibabu, kulingana na hati zilizoonekana na RFI.

Lakini mbali na maabara, vikwazo vingine viwili vinaendelea kuzuia uelewa sahihi wa hali ya ugonjwa: upinzani wa jamii kuorodhesha na kufuatilia watu waliotangamana na wagonjwa waliothibitishwa, kama ilivyo katika eneo la afya la Fizi, kama kilomita ishirini kutoka Bunia; na ripoti ndogo ya tahadhari kutoka maeneo ya afya katika mikoa mitatu yaliyoathiriwa. Hata hivyo, arifa hizi ni kiungo muhimu katika mapambano dhidi ya virusi, kwa sababu zisipotolewa haraka, uthibitisho wa visa vinavyowezekana vya maambukizi unajikokota, na huduma kwa wagonjwa inatolewa kwa mwendo wa kinyonga pia, anaeleza mjumbe wa timu ya kukabiliana mlipuko wa virusi vya Ebola.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii