Urusi na Ukraine zimeendelea kushambuliana vikali usiku kucha kwa kutumia droni na makombora. Mapigano hayo yanaonesha kuendelea kwa mvutano mkali kati ya pande hizo licha ya juhudi za kimataifa za kupunguza vita.
Kwa mujibu wa taarifa nchini humo mji wa bandari wa kusini mwa Urusi
wa Taganrog uliopo katika Bahari ya Azov watu wawili wamejeruhiwa ambapo Meya wa
mji huo Svetlana Kambulova amesema kupitia mtandao wa Telegram kuwa majeruhi
hao wamepelekwa hospitalini.
Kwa mujibu wa tovuti huru ya mtandaoni ya Astra, kiwanda cha
ukarabati wa ndege kililengwa katika shambulio hilo pia mashambulizi
yameripotiwa katika maeneo ya Tuapse, Voronezh na Crimea.
Katika eneo la Crimea ambalo
lilinyakuliwa na Urusi mwaka 2014, milipuko imeripotiwa katika mji mkuu
Simferopol pamoja na bandari ya kijeshi ya Sevastopol.
Mapigano hayo yanaonesha kuendelea kwa mvutano mkali kati ya pande hizo mbili licha ya juhudi za kimataifa za kupunguza vita vya Ukraine .
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime