Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 11.12.2021

Real Madrid wanafuatilia hali ya Cristiano Ronaldo katika klabu ya Manchester United. Klabu hiyo ya La Liga inaamini kuwa mkataba wa mshambuliaji huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 36 unaweza kusitishwa mwezi Januari kufuatia kuwasili kwa Ralf Rangnick Old Trafford. (Football Insider)

Meneja wa muda wa Manchester United Rangnick ameishauri klabu hiyo kufuatilia kiungo wa kati wa RB Leipzig na Mali Amadou Haidara, 23, kiungo wa kati wa Borussia Dortmund Muingereza Jude Bellingham, 18, na kiungo wa kati wa Leeds United na England Kalvin Phillips, 26. (ESPN)

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii