Kesi dhidi ya bin Salman kuhusu mauaji ya Khashoggi yafutwa

Jaji mmoja nchini Marekani ameitupilia mbali kesi dhidi ya Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman kuhusiana na mauaji ya mwaka wa 2018 ya mwandishi habari Jamal Khashoggi.

Jaji John Bates amezungumzia kile alichokiita wasiwasi kuhusiana na uamuzi wake lakini akasema ilimbidi kufuata pendekezo la karibuni la Wizara ya Sheria ya Marekani kuwa bin Salman apewe kinga ya kushitakiwa. Wasiwasi wa Bates ulitokana sio tu na tuhuma za kuaminika za kuhusika kwa mwanamfalme huyo katika mauaji ya Khashoggi, lakini pia na wakati wa uteuzi wa bin Salman kuwa waziri mkuu wa Saudi Arabia. Kesi hiyo iliwasilishwa na mchumba wa Khashoggi, Hatice Cengiz, ambaye anamtuhumu Rais wa Marekani Joe Biden kwa kumpa kinga bin Salman.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii