Katika kusaidia juhudi za maafa baada ya tetemeko kubwa la ardhi ambalo limesababisha vifo vya watu zaidi ya 3,000, na maelfu kadhaa kujeruhiwa, nchi ya Sudan imetuma timu ya watu 40 ya utafutaji na uokoaji nchini Uturuki.
Jeshi la Polisi nchini humo, kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, timu ya wanachama wakiwemo wafanyakazi 7 wa Kikosi cha Ulinzi wa Wananchi waliondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Khartoum kueleke Gaziantep Ijumaa asubuhi ya Februari 10, 2023.