Dkt. Mpango akemea mamlaka za maji kuzoea matatizo ya Wananchi

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango amewataka Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kutumia Mitambo ya uchimbaji visima ilionunuliwa na serikali kwa matumizi yaliokusudiwa ikiwemo kutoa huduma kwa wananchi kwa gharama nafuu na kuacha tabia ya kuzoea matatizo ya Wananchi bali wayatatue kwa weledi.

Dkt. Mpango amesema hayo wakati akikagua magari na mitambo ya uchimbaji visima na mabwawa yaliokabidhiwa kwa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Taarifa ya Utendaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira kwa mwaka 2021/2022 iliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam leo Machi 20, 2023.

Amesema, serikali inaendelea kutafuta njia bora na fupi zaidi katika utoaji wa msamaha wa kodi ili kuharakisha utekelezaji wa miradi mbalimbali hapa nchini ikiwemo miradi ya maji na kukemea mitambo hiyo kutumika kwa matumizi binafsi, huku akiiagiza RUWASA kutoa huduma zaidi kwa wananchi kuliko kufanya biashara.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii