Muungano wa Azimio umevumbua mtandao utakaotumika kuhifadhi picha za matukio ya maandamano yanayotarajiwa kufanyika kila Jumatatu na Alhamisi.
Kiongozi wa wachache katika bunge la taifa Opiyo Wandai amesema kuwa uvumbuzi wa mtandao huo uliafikiwa baada ya serikali kuonekana kutaka kutatiza uhuru wa vyombo vya habari.