Daktari wa Marekani apona Ebola nchini Ujerumani wakati wagonjwa 488 wakiripotiwa DRC

Daktari wa Marekani, ambaye aliambukizwa virusi Ebola alipokuwa akifanya kazi nchini DRC, amepona baada ya matibabu ya zaidi ya wiki mbili nchini Ujerumani, kulingana na hospitali iliyompokea.

Hospitali ya umma ya Charité ya Berlin imesema mtu huyo, aliyetambuliwa kwenye vyombo vya habari kama Peter Stafford mwenye umri wa miaka 39, yuko katika "afya njema" na aliruhusiwa kutoka karantini siku ya Jumamosi.

Stafford, ambaye alifanya kazi kama daktari wa upasuaji wa kundi la wamisionari wa Kikristo nchini DRC, alilazwa Mei 20 baada ya kipimo kufichua kwamba alikuwa na virusi vya Bundibugyo, aina ya Ebola iliyotambuliwa wakati wa mlipuko huo Afrika Mashariki na Kati. Inaaminika aliambukizwa virusi hivyo alipokuwa akimfanyia upasuaji mgonjwa wa Ebola mashariki mwa DRC, kabla ya mlipuko huo kutangazwa rasmi nchini humo mnamo Mei 15.

Stafford alisafirishwa kutoka Uganda hadi Berlin kwa ndege maalum na kulazwa katika hospitali ya Charité chini ya masharti makali ya usalama.

Mkewe na watoto wake wanne, ambao hawakuwa na dalili za ugonjwa lakini mwanzoni walichukuliwa kuwa "watu walio katika hatari kubwa ya kuambukizwa," walifika Berlin muda mfupi baadaye na kuwekwa karantini katika sehemu tofauti ya wodi. Kutengwa kwao kuliondolewa Jumamosi.

Ingawa chanjo tatu zinaendelea kutengenezwa na zinatarajiwa kufanyiwa mchakato wa majaribio ya kliniki ulioharakishwa, hakuna chanjo ambayo bado imeidhinishwa kwa virusi vya Ebola, aina ya Bundibugyo.

Kulingana na taarifa kutoka hospitalini, Stafford amesema alipata matibabu ambayo yalijumuisha "matibabu ya majaribio ambayo kwa sasa yanajaribiwa kwa aina hii ya virusi."

Ameushukuru uongozi wa hospitali na wafanyakazi, akisema kwamba "maneno hayatoshi kuelezea shukrani zangu," na akaongeza: "Tunafikiri tu Wakongo ambao hawana huduma kama hii."

Leif Erik Sander, mkurugenzi wa magonjwa ya kuambukiza na kitengo cha wagonjwa mahututi cha hospitali hiyo, ameelezea kupona kwa mgonjwa huyo kama "mafanikio makubwa ya kimatibabu."

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii