Unafikiri ni kwanini Taifa Stars haifanyi vizuri Kimataifa tangu mwaka 1980 hizi hapa sababu

Tangu miaka ya 1980 Taifa stars imekuwa ikipambana kupata mafanikio makubwa kimataifa.

Ambapo tatizo si wachezaji kukosa kipaji,bali ni mfumo mzima wa soka nchini kuwa na changamoto.

Matatizo  makuu:

1: Ukosefu wa uwekezaji wa kutosha.

* Nchi kama Morocco na South Africa zimewekeza kwenye viwanja vya kisasa,academy na sayansi ya michezo.

* mfano,Morocco ilianzisha akademi ya mohamed VI football Academy na sasa inazalisha wachezaji wa kimataifa kama Hakim Ziyech.

2:Ligi ya ndani kutokuwa imara vya kutosha.

* Ligi imara huzalisha timu ya taifa imara.

* mfano: Egypt inaligi yenye ushindani na uwekezaji matokeo yake Taifa lao limetwaa AFCON mara 7.

3: Academy  chache na kukosa mfumo wa kuibua vipaji mapema.

* Nchi kama Senegal limefanikiwa kupitia Academy za mpira.

* Mfano: Generation football Academy ilimzalisha Sadio Mane,aliyekuwa nyota wa Liverpool na Bayern. 

4.Maandalizi hafifu kabla ya mashindano .

* Timu nyingi za Afrika magharibi huanza kambi miezi kadhaa kabla ya mashindano.

* Mfano: Senegal hucheza mechi nyingi za kirafiki dhidi ya timu kubwa kama Brazil na Algeria kabla ya mashindano.

5: Kukosa mwendelezo wa sera na mipango.

* Kila kocha au uongozi ukija huanza upya badala ya kuendeleza alipoishia mwenzake.

Nini kifanyike ?(Suluhisho).

1: Uwekezaji kwenye miundo mbinu.

* Kujenga Academy za soka kila kanda kama ilivyofanya Senegal na Morocco.

2:Kuboresha ligi ya ndani.

* Kuongeza udhamini,usimamizi,na kutumia teknolojia(VAR,data analysis).

3: Kuanzisha mpango wa  taifa wa kuendeleza vipaji.

* Vipaji viibuliwe mashuleni kuanzia umri wa miaka 12 hadi 17.

4. Kuongeza mechi za kimataifa za kirafiki.

* Mfano kucheza na timu bora ili kuongeza  uzoefu.

* mfano:Japan iliboresha soka lake kwa kucheza na Brazil ,German na ufaransa mara kwa mara kabla ya kuwa na mafanikio.

5:Kutumia sayansi ya michezo.

*Fitness ,psychology,nutrition,performance analysis.

6:Kuwa na sera ya muda mrefu (10 to 15 years plan).

* Isibadilike kwa kubadilika kwa kocha au viongozi.

Taifa stars haijakwama kwa kukosa vipaji,bali kwa mfumo usiowezesha vipaji kustawi. 

Tukiboresha Academy,  ligi , maandalizi na uwekezaji tunaweza kuona mafanikio kama ya Morocco, Senegal na Egypt.

Na: Mbeki Mbeki.

Kagera.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii